Sunday, 14 September 2014

Je, Afrika Kusini ni ‘Nchi Iliyokwama'? Ndivyo Alan Dershorwitz Anavyofikiri

Waafrika Kusini wamekuja juu kuitetea nchi yao baada ya mwanasheria wa Kimarekani na mchambuzi wa duru za kisiasa Alan Dershorwitz kuiita Afrika Kusini kuwa ni “nchi iliyokwama “ wakati akijadili mashitaka ya mauaji ya  Oscar Pistorius  kwenye kipindi cha Piers Morgan kwenye chaneli ya habari ya CNN.
Mwanariadha huyo wa Afrika Kusini asiye na miguu yote miwili  alimpiga risasi na kumwuua rafiki yake wa kike Reeva Steenkamp mnamo Februari 14, 2013; bingwa huyo wa mashindano ya Olimpiki anadai kuwa alidhani anamwuua mtu mhalifu aliyevamia nyumba yake.
American lawyer and political commentator Alan Dershowitz. Photo released under Creative Commons by Flickr user The Huntington.
Mwanasheria wa Marekani na mchambuzi wa mambo ya kisiasa Alan Dershowitz. Picha imetolewa kwa haki miliki ya Creative Commons na mtumiaji wa Flickr aitwaye The Huntington.
Dershorwitz alitoa maoni kwenye mahojiano , “Nimekaa kidogo nchini Afrika Kusini hivi karibuni, na watu hawataki kusikia hili, lakini Afrika Kusini ni nchi iliyokwama.”
Mtazame Dershowitz akitoa matamshi hayo hapa chini:
Muda mfupi baadae, wataalamu wa Uchumi nchini Afrika Kusini walijitokeza kukanusha matamashi hayo, wakisema kuwa nchi ya Afrika Kusini haina vigezo vyovyote vya kuitwa “taifa lililokwama kiuchumi” kama vile ghasia zilizoenea za wenyewe kwa wenyewe, kutokufanya kazi kwa asasi za kiraia, kutokuwepo kwa mhimili wa mahakama unaojitegemea na kutokuwepo kwa ulinzi wa mali za watu.
Waafrika Kusini waliingia kwneye mtandao wa Twita kuonyesha hasira zao na kukana kabisa madai hayo

WHO yatiwa wasiwasi na kusambaa kwa virusi vya Ebola Afrika

Madaktari wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka MSF wanabeba muili wa mtu aliefariki kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mji wa Guékédou, nchini Guinea, Aprili 01 mwaka 2014.
Madaktari wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka MSF wanabeba muili wa mtu aliefariki kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mji wa Guékédou, nchini Guinea, Aprili 01 mwaka 2014.
AFP PHOTO / SEYLLOU

Mataifa ya Afrika yajidhatiti kwa kupambana dhidi ya Homa ya Ebola

Shirika la madaktari wasio na mipaka likiendelea kupokea watu wanaoambukizwa virusi vya Ebola,  katika kijiji cha Kailahun, nchini Sierra Leone.
Shirika la madaktari wasio na mipaka likiendelea kupokea watu wanaoambukizwa virusi vya Ebola, katika kijiji cha Kailahun, nchini Sierra Leone.
REUTERS/Tommy Trenchard

Mtuhumiwa wa mauaji ya watawa watatu wa kiitaliano huko Burundi akamatwa, DRC-katibu Mkuu wa chama cha UNC ahukumiwa mwaka mmoja Jela


 

Iraq: baraza la mawaziri latangazwa, Marekani yapongeza



Waziri mkuu mpya wa Iraq, Haidar Al Abadi akiwa Bungeni mjini Baghdad, nchini Iraq.
Waziri mkuu mpya wa Iraq, Haidar Al Abadi akiwa Bungeni mjini Baghdad, nchini Iraq.

Na kennedyrutta
Waziri wa mambo ya nje wa marekani john Kerry amelikaribisha baraza jipya la mawaziri lililotangazwa jana juma tatu nchini Iraq, na kusema kuwa baraza hilo litaleta mustakabali wa taifa hilo.

Waziri Mkuu Haidar al Abadi, amewaambia waandishi wa habari kuwa huenda serikali hiyo ikasababisha nchi yake kuondokana na makundi ya wapiganaji wanaotishia usalama wa taifa hilo, endapo kutakuwa na kuaminiana miongoni mwa wananchi.
Hata hivyo hakuna Waziri wa ulinzi wala wa mambo ya ndani ya nchi aliyetangazwa mpaka sasa. Lakini waziri mkuu wa nchi hiyo amesema atafanya uteuzi wa mawaziri hao kwa muda wa wiki moja.
Akisisitizia msimamo wa Marekani, waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry amesema kwamba serikali yake itashirikiana kwa karibu na serikali hiyo.
Nafasi nyingine za mawaziri zimejazwa kwa mujibu wa makubaliano kati ya Washia walio wengi, Wasunni hali kadhalika na Wakurd walio wachache.

Shirika la kutetea Haki za binadamu la Human Rights lawatuhumu wanajeshi wa AMISON kuhusika na Ubakaji nchini Somalia.

Jumatano 10 septemba 2014

 
Na kennedyrutta
Ripoti iliyotolewa na shirika la kimataifa la Human Rights Watch imewatuhumu askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika huko Somalia AMISOM, kuhusika na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, wanawarubuni wanawake kwa kuwapa chakula kama msaada ili wafanye nao ngono, tuhma ambazo AMISOM imekanusha.

Afrika Kusini: Oscar Pistorius aendelea kunufaika na dhamana Mahakama yafuta tuhuma ya mauaji iliyokua inamkabili mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, Septemba 11 mwaka 2014. Mahakama yafuta tuhuma ya mauaji iliyokua inamkabili mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, Septemba 11 mwaka 2014. REUTERS/Siphiwe Sibeko Na RFI Kwa mujibu wa jaji wa mahakama ya mji wa Pretoria nchini Afrika Kusini, Thokozile Masipa, Oscar Pistorius hana hatia ya kumuua Reeva Steenkamp, mauaji ambayo yalitokea Februari 14 mwaka 2013. Hata hivo haimaanishi kuwa mwanariadha huyo hatohukumiwa. Tangazo hilo limetolewa alhamisi wiki hii mchana : Jaji amebaini kwamba Oscar Oscar Pistorius alimfyatulia risase mpenzi wake Reeva Steenkamp kupitia mlango huu. REUTERS/Alexander Joe/Pool hana hatia ya mauaji. Kwa kutetea uamzi wake, hakimu huyo ameeleza kwamba kuna tofauti kati ya kufyatua risase na kuwa na nia ya kuua. Je mwanariadha huyo alikua na nia ya kuua mpenzi wake wakati alipofyatua risase kwenye mlango wa choo? Mwanariadha alikanusha mwenyewe na kusema kwamba alifyatua risase kwenye mlango wa choo baada ya kusikia mtu chooni akidhani kwamba ni mtu ambaye alikua amekuja kuhatarisha usalama wake. Mku wa kikosi cha usalama nchini Arfika kusini, Pieter Baba, akitoa ushahidi wake katika kesi ya Oscar Pistorius, mjini Pretoria, Machi 07 mwaka2014. REUTERS/Schalk van Zuydam/Pool Maswali yote yako wazi, je alikua na dhamira ya kuua? Jaji, Thokozile Masipa, amebaini hapana, kwa sababu ya mwenendo wake aliyouonesha muda mfupi baada ya tukio hilo : alipigia sim vyombo vya usalama, wakati huo huo alimpigia sim daktari ili aweze kuwasili eneo la tukio na kumfanyia matibabu mpenzi wake huyo wa zamani ambaye alimfyatuliwa risase bila kukusudia. Muda mchache uliyofuata, alibaini kwamba alikua alijidanganya, hakua na nia ya kumuua. Jaji amesema kutokana na hali ya uzuni aliyokua nayo, Oscar hangelikumbuka katika utetezi wake kusema yote aliyoyafanya akijaribu kuokoa maisha ya Reeva Steenkamp. Kutokana na utetezi wake, Oscar Pistorius hakupatikana na hatia yakuua kwa kukusudia. Saa moja kabla, jaji alitupilia mbali hoja ya kuua bila kukusudia iliyotolewa na mwendeshamashtaka dhidi ya Oscar. Kinachosalia kwa sasa ni hukumu dhidi ya kuua bila kukusudia au kuachiliwa huru. Lakini hata hivo, sheria ya jinai ya Afrika Kusini haiweki wazi hukumu ya kosa la kuua bila kukusudia. Hukumu imetolewa, lakini huenda Pistorius akapewa adhabu ya kufungwa jela au adhabu ya kifungo jela ikiwa ni pamoja na faini. Jaji Thokozile Masipa amesema adhabu hiyo itatolea Oktoba 13 mwaka 2014. Jaji Masipa ametupilia mbali ombi la mashtaka la kutaka dhamana ya Pistorius ibatilishwe, na kubaini kwamba upande wa mashtaka haukuonesha umuhimu wowote wa kubatilisha dhamana hiyo na badala yake ameongeza muda hadi pale uamzi wa adhabu urtakapochukuliwa. Wakati hakimu alipotangaza kufuta tuhuma ya mauaji, Pistorius ameangua kiliyo, huku akitokwa na machozi mengi kizimbani. Oscar Pistorius mwanariadha aneishi na ulemavu.

Afrika Kusini: Oscar Pistorius aendelea kunufaika na dhamana

Mahakama yafuta tuhuma ya mauaji iliyokua inamkabili mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, Septemba 11 mwaka 2014.
Mahakama yafuta tuhuma ya mauaji iliyokua inamkabili mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius, Septemba 11 mwaka 2014.
REUTERS/Siphiwe Sibeko

Na kennedyrutta
Kwa mujibu wa jaji wa mahakama ya mji wa Pretoria nchini Afrika Kusini, Thokozile Masipa, Oscar Pistorius hana hatia ya kumuua Reeva Steenkamp, mauaji ambayo yalitokea Februari 14 mwaka 2013. Hata hivo haimaanishi kuwa mwanariadha huyo hatohukumiwa.

Tangazo hilo limetolewa alhamisi wiki hii mchana : Jaji amebaini kwamba Oscar

Oscar Pistorius alimfyatulia risase mpenzi wake Reeva Steenkamp kupitia mlango huu.
REUTERS/Alexander Joe/Pool
hana hatia ya mauaji. Kwa kutetea uamzi wake, hakimu huyo ameeleza kwamba kuna tofauti kati ya kufyatua risase na kuwa na nia ya kuua. Je mwanariadha huyo alikua na nia ya kuua mpenzi wake wakati alipofyatua risase kwenye mlango

Burundi : chama tawala na utawala wa Bujumbura vyanyooshewa kidole

Amnesty International yanyooshea kidole chama tawala Cndd-Fdd na serikali ya Bujumbura kwa vitisho dhidi ya upinzani na mashirika ya kiraia.
Amnesty International yanyooshea kidole chama tawala Cndd-Fdd na serikali ya Bujumbura kwa vitisho dhidi ya upinzani na mashirika ya kiraia.

Burundi: Pierre Nkurunziza awonya baadhi ya wanasiasa



Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza.
REUTERS/Stringer

Na kennedyrutta
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, jumanne wiki hii,

Raia watatu wa Italia wauawa nchini Burundi

Kanisa kuu la Katoliki mjini Bujumbura (Burundi).
Kanisa kuu la Katoliki mjini Bujumbura (Burundi).
flickr

Na kennedyrutta
Watawa watatu, raia wa Italia, wameuawa kikatili usiku wa jumapili kuamkia jumatatu wiki hii katika makaazi yao wilayani Kamenge katika manispa ya jiji la Bujumbura nchini Burundi, vyanzo vya utawala na polisi vimeeleza.

Kwa mujibu wa viongozi wa Italia, marehemu hao, Olga Raschietti, mwenye umri wa miaka 83 na Lucia Pulici, mwenye umri wa miaka 75, ni kutoka jamii ya wamisionari wa kanisa Katoliki, ambao makaazi yao ni wilayani Kamenge, kaskazini mashariki mwa mji wa Bujumbura. Maiti nyingine ya tatu imeokotwa mapema jumatatu alfajiri wiki hii kati ya saa tisa na saa kumi karibu na eneo walikouawa wenziye.
Watawa hao wamekua wakiishi katika eneo la kanisa Katoliki la parukiya ya Guido Maria Conforti. Kiongozi wa wilaya ya Kamenge Damien Baseka amebaini kwamba watawa hao wameuawa kikatili.
“ Mtuhumiwa ni kijana wa kiume, ambaye alionekana, akikimbia baada ya kutekeleza kitendo hicho kiovu saa kumi na moja jioni”, amesema Baseka.
Afisa mmoja wa polisi, ambaye hakupendelea jina lake litajwe, ameeleza kwamba watawa hao walikatwa vichwa, kabla ya mmoja wao kupigwa mawe usoni.
Kwa mujibu wa dayosisi ya Parma, nchini Italia, ambayo imerusha hewani picha za watawa hao wakivalia nguo za kawaida, nyuso zao zikiwa zimekunjika kutokana na uzee, wanadini hao wameuawa wakati wa jaribio la wizi lililokua likiendeshwa na kijana mmoja, bila hatahivo kutajwa jina lake.
Kwa mujibu wa afisa mmoja mwandamizi wa polisi nchini Burundi, kulingana na uchunguzi wa mwanzo, wizi huo si sababu ya kitendo hicho kivu.
" Mhalifu huyo hakuiba chochote hata pesa ziliyokua eneo la tukio hakubeba (...). Tumeanza kumtafuta muhusika, ambaye amejulikana, baada ya uchunguzi wetu”, ameseama afisa huyo wa polisi.
Mwezi Novemba mwaka 2011, mtawa raia wa Italia pamoja na raia wa Croatia waliuawa kwa risase wakiwa katika shughuli yao ya kidini katika mkoa wa Ngozi, kaskazini mwa Burundi. Vijana wawili walikamatwa, baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji hayo. Vijana hao walihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kesi yao kuharakishwa.

Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, rais wa

 
Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, rais wa Rwanda, Paul Kagame (kushoto) na rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni (kulia).
 Rwanda, Paul Kagame (kushoto) na rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni (kulia).
Reuters
Na kennedyrutta
Makala haya ya Afrika ya Mashariki inaangaziajuu ya hati za kusafiria kwa raia wa afrika ya mashariki. Nchi za Kenya, Rwanda na Uganda zimekubaliana kutumia vitambulisho vya uraia kutoka nchi moja hadi nyingine baina ya nchi hizo. Je, kuna changamoto gani katika utekelezwaji wa hatua hiyo? Kujua mengi zaidi, sikiliza makala haya.

Timu Kenya kukusanya mafanikio muhimu katika fundraiser mechi



  Imesasishwa 12/09/14 | Kwa MICHEZOAFRIKA


Ilikuwa jioni ya msisimko katika Nyayo uwanja wa mpira wa kikapu gymnasium kama timu ya taifa wanaume na wanawake zilizokusanywa mafanikio muhimu katika kujenga yao juu kabla ya mechi ujao michuano ya mpira wa kikapu Eneo la 5 kuwa mwenyeji katika Kampala Uganda.

Mwanariadha Oscar Pistorius Apatikana Na Hatia Ya Kumuua Mpenzi wake Bila Kukusudia.



JajiThokozile Masipaal anayeendasha kesi ya Oscar amesema mwanariadha huyu alimmuampenzi wake Reeva Steenkamp kwa bahati mbaya na upande wa mshtaka umeshindwa kuthibitisha Oscar alikusudia kuua.
Oscar amepatikana na kosa la kutumia silaha yake visivyo kwenye mgahawa fulani mjini Johannesburg. Sababu atahukumiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia atakaa jela kwa muda mfupi zaidi na sheria za Afrika Kusini wanasema sio zaidi ya miaka 15

Marekani vitani dhidi ya IS




F-35 Kampfflugzeug
Ndege za kijeshi za Marekani zinashambulia maeneo ya wanamgambo nchini Iraq
Katika mahojiano kadhaa ya televisheni waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry ameonekana kusita kutamka kuhusu operesheni zilizopanuliwa za Marekani dhidi ya kundi la IS nchini Iraq na Syria kuwa ni "vita"

Shearer asema Welbeck atang'ara Arsenal



.

Mshambuliaji mpya wa kilabu yaArsenal Danny Welbeck anaweza kufunga mabao 25 kwa msimu mmoja ,hayo ni matamshi ya aliyekuwa mshambuliaji wa England Allan Shearer.
Wellbeck mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na kikosi cha The Gunners kutoka kilabu ya Manchester United kwa kitita cha pauni millioni 16 katika siku ya mwisho ya dirisha la kuwasajili wachezaji wa soka barani ulaya na anaweza kuanzishwa kwa mara ya kwanza dhidi ya watetezi wa ligi hiyo Manchester City siku ya jumamosi.
Nimesikia watu wakisema kwamba Wellbeck hawezi kufunga mabao 20 ama 25 kwa msimu mmoja ,sikubaliani na hilo Shearer.
''Sasa ana uwezo wa kuonyesha umahiri wake katika ligi hiyo.''.
Siku ya Alhamisi Meneja wa kilabu ya Manchester United Van Gaal alisema kuwa Wellbeck hakuweza kufunga mabao ya kutosha wakati alipkuwa katika kilabu hiyo ya Old Trafford.
Mshambuliaji huyo ambaye ni mzaliwa wa Manchester ambaye aliifunga mabao yote mawili timu ya Uingereza dhidi ya Switzerland siku ya jumatatu ,hajawahi kufunga zaidi ya mabao tisa katika ligi ya Uingereza tangu alipoanza kuchezea mwaka 2008.

Uganda yatibua shambulizi la kigaid




Maafisa wa polisi nchini Uganda wameimarisha usalama katika maeneo mengi ya uma katika mji mkuu wa Kampala kufuatia kukamatwa kwa washukiwa kadhaa wa makundi ya kigaidi na vilipuzi

Monday, 8 September 2014

Je, Afrika iko tayari kuushinda ugaidi?

mjusi blogspot.com

Licha ya viongozi wa Kiafrika kukutana jijini Nairobi kuzungumzia mikakati ya kupambana na ugaidi, wasiwasi uliopo ni ikiwa kweli Afrika iko tayari kukabiliana na tatizo hili la kimataifa.
Mkutano wa viongozi wa Afrika juu ya ugaidi jijini Nairobi. Mkutano wa viongozi wa Afrika juu ya ugaidi jijini Nairobi.
Tarehe 21 Septemba 2013 wanamgambo wa al-Shabaab walilivamia jengo la maduka la Westgate jijini Nairobi, Kenya, ambako waliwauwa watu zaidi ya 60, huku ikivichukuwa vyombo vya usalama vya nchi hiyo siku nne kuukomeshwa mzingiro wa jengo hilo. Mwaka mmoja baadaye, taarifa za uhakika juu ya namna tukio hilo lilivyotokea - kama vile idadi ya washiriki na njia zilizotumika - bado hazijapatikana.
Kisha baina ya tarehe 14 na 17 Juni 2014, wanamgambo wakavamia kijiji cha Mpeketoni, Kaunti ya Lamu, na tena wakawauwa watu zaidi ya 60. Bila ya shaka, orodha ya mauaji mengine yenye sura kama hiyo imekuwa ikiendelea.
Aprili 2014, kundi la Boko Haram liliwateka nyara wasichana 276 kutoka kijiji cha Chibok, jimboni Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria. Hadi sasa, Boko Haram imeshateka watu wengine kadhaa na huku wengi wa waliowateka awali wakiwa bado mikononi mwao.
Mwili wa mmoja wa waliouawa kwenye mashambulizi ya Mpeketoni. Mwili wa mmoja wa waliouawa kwenye mashambulizi ya Mpeketoni.
Mwanzoni mwa Septemba 2014, viongozi wa Afrika walikutana jijini Nairobi, Kenya, kuujadili ugaidi, ambapo mwenyeji wao, Rais Uhuru Kenyatta, aliwaambia wenzake ugaidi Afrika ni uhalisia sasa.
"Ni jambo la kutia wasiwasi barani Afrika hivi leo kuona namna makundi ya kigaidi yalivyoongezeka kwa idadi na kwa uwezo. Boko Haram inaendelea kuzitia mashakani sehemu za mataifa ya Nigeria, Chad na Cameroon kwa mbinu mpya, kama vile kuwateka nyara wasichana 200 hivi karibuni, pia tuna al-Qaida tawi la Maghreb." Alisema Kenyatta kwenye mkutano huo.
Ugaidi ndio mada yetu leo Mbele ya Meza ya Duara, tukiangalia uzito wa kitisho hiki, athari zake na, kubwa kuliko yote, uhalisia wake na uwezo wa bara la Afrika kukabiliana nao. Kaskazini, eneo liitwalo Sahel, kuna tawi la al-Qaida la Maghreb, magharibi kuna Boko Haram, mashariki kuna al-Shabaab, na kama alivyosema Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria kwenye mkutano huo wa Nairobi, kitisho hiki kinavuuka makundi moja moja tu, na kuwa muunganiko wa makundi mengine kadhaa ya kihalifu na kigaidi kwa pamoja.
"Kitisho hiki kinakuwa changamano zaidi kwa kukuwa kwa mafungamano kati ya ugaidi na uhalifu wa kupangwa wa kimataifa, hasa hasa madawa ya kulevya na magendo ya silaha, biashara haramu ya binaadamu, na utakatishaji fedha zinazopatikana kwa njia haramu."
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Kwa mujibu wa Rais Idriss Deby wa Chad, ambaye ndiye mwenyekiti wa sasa wa Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika, mkutano huo wa Nairobi ulizungumzia uwezekano wa kuwa na mfuko wa pamoja kupambana na ugaidi barani Afrika.
Lakini je, hilo kweli linawezekana? Je, Afrika inaweza kupambana na ugaidi kwa nguvu na uwezo wake wote, kiwango ambacho inakabiliana na mengine? Je, mkutano huu wa Nairobi ulikuja wakati tayari umeshachelewa? Juu ya yote, sababu za ugaidi barani Afrika ni zipi?
Kuchambua mada hii, Mohammed Khelef anaongoza majadiliano kati ya Maggid Mjengwa, ambaye ni mwandishi wa habari, mchambuzi wa siasa za Afrika na mwanaharakati akiwa Iringa, Tanzania; Ally Saleh, ambaye ni mwanasheria, mwandishi wa habari wa kimataifa na pia mwanaharakati wa haki za binaadamu, Zanzibar, na Werunga Simiyu, mchambuzi wa masuala ya usalama kutoka Nakuru, Kenya.

upizani wa vyama vya siasa nchini Kongo juu ya kufanyiwa marekebisho katibaupizani wa vyama vya siasa nchini Kongo juu ya kufanyiwa marekebisho katiba



·          

Kwa mara nyingine tena chama cha 'Mrengo wa Kitaifa kwa ajili ya Marekebisho' nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kimesisitiza kuwa hatua ya kuifanyia marekebisho ya katiba ya nchi hiyo ina maana ya kuibua machafuko nchini. Viongozi wa chama hicho kwa kushirikiana na vyama vingine vya upinzani nchini Kongo wamelaani njama zozote za kutaka kutekeleza jambo hilo. Kabla ya hapo chama kilichoungana na chama tawala cha 'Wananchi kwa ajili ya Marekebisho na Demokrasia' kilitangaza azma ya kuifanyia marekebisho katiba ya Kongo. Kwa mujibu wa habari, marekebisho hayo yatahusu kipengee cha 220 ambapo ikiwa hatua hiyo itaungwa mkono na wananchi katika kura ya maoni, basi itatoa fursa kwa Rais Joseph Kabila kugombea kwa mara ya tatu katika uchaguzi mkuu ujao. Rais Kabila ambaye alichukua uongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuuawa baba yake Laurent-Désiré Kabila hapo mwezi Juni mwaka 2001, alishinda katika uchaguzi wa mwaka 2006 na 2011.

Leo ni Jumatatu tarehe 12 Mfunguo Pili Dhil-qaad mwaka 1435 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 8 Septemba mwaka 2014 Miladia.



  •  

 Siku kama ya leo miaka 36 iliyopita, wanajeshi wa utawala wa kidikteta wa Pahlavi walisambaratisha maandamano makubwa ya wananchi wa mji wa Tehran nchini Iran. Wananchi Waislamu wakazi wa Tehran siku hiyo walianza kuandamana tangu asubuhi, hayo yakiwa maandamano ya siku kadhaa mfululizo kuwahi kufanywa na wakazi wa mji wa Tehran dhidi ya utawala wa kibaraka wa Pahlavi. Wakati huo, utawala wa kijeshi ulikuwa umetangazwa katika mji wa Tehran, lakini wananchi Waislamu bila ya kuzingatia hali hiyo, wakamiminika mitaani wakipiga nara dhidi ya utawala wa Shah. Wakati huo huo walinzi maalumu wa Shah walifanya mashambulizi na katika muda mfupi wakawaua shahidi wananchi zaidi ya elfu nne wa Tehran waliokuwa wakipigania haki zao.

Alshabaab wamteua kiongozi mpya




Kiongozi huyo mpya ni Ahmad Umar ambaye hajulikani sana. Mmoja wa makomandawa Al Shabaab Abu Mohammed, alisema uamuzi wa kumteua kiongozi huyo ulifikiwa bila pingamizi.
  • http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/01a5bf934eaed0c12b6cbc6810e1ab64_XL.jpg

Serena Williams bingwa US Open