Monday, 8 September 2014

Leo ni Jumatatu tarehe 12 Mfunguo Pili Dhil-qaad mwaka 1435 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 8 Septemba mwaka 2014 Miladia.



  •  

 Siku kama ya leo miaka 36 iliyopita, wanajeshi wa utawala wa kidikteta wa Pahlavi walisambaratisha maandamano makubwa ya wananchi wa mji wa Tehran nchini Iran. Wananchi Waislamu wakazi wa Tehran siku hiyo walianza kuandamana tangu asubuhi, hayo yakiwa maandamano ya siku kadhaa mfululizo kuwahi kufanywa na wakazi wa mji wa Tehran dhidi ya utawala wa kibaraka wa Pahlavi. Wakati huo, utawala wa kijeshi ulikuwa umetangazwa katika mji wa Tehran, lakini wananchi Waislamu bila ya kuzingatia hali hiyo, wakamiminika mitaani wakipiga nara dhidi ya utawala wa Shah. Wakati huo huo walinzi maalumu wa Shah walifanya mashambulizi na katika muda mfupi wakawaua shahidi wananchi zaidi ya elfu nne wa Tehran waliokuwa wakipigania haki zao.

Miaka 60 iliyopita katika siku kama ya leo, mkataba wa SEATO wa makubaliano ya kiulinzi ya Asia ya Kusini-Mashariki ulisainiwa katika mji mkuu wa Ufilipino, Manila. Serikali za Marekani, Uingereza, Australia, Pakistan, Thailand, Ufaransa, New Zealand na Ufilipino ndizo zilizosaini mkataba huo. Nchi hizo zilikubaliana kusaidiana iwapo zingeshambuliwa na nchi nyingine au kukabiliwa na uasi wa ndani.
Miaka 91 na katika siku kama ya leo, sawa na tarehe 12 Dhil Qaada mwaka 1344 Hijiria, alifariki dunia Adib Neishabur, mshairi maarufu wa Iran. Neishabur alizaliwa mwaka 1281 Hijiria katika mji wa Neishabur kaskazini mwa Iran, na utotoni mwake alipatwa na maradhi ya tete kuwanga yaliyompelekea kuwa kipofu. Lakini suala hilo halikumrudisha nyuma na kwa jitihada nyingi alijishughulisha kutafuta elimu na kuwa mahiri katika fasihi ya Kiarabu na Kifarsi. Katika maisha yake, Neishabur alijishughulisha na utunzi wa mashairi na kuandika vitabu vingi katika uwanja huo.
 Na miaka 73 iliyopita muwafaka na leo, wanajeshi wa Ujerumani ya Kinazi waliuzingira mji wa Leningrad, Saint Petersburg ya sasa. Hata hivyo mji huo haukutekwa na jeshi la Kinazi, licha ya utabiri wa Adolf Hitler na makamanda wake. Wakazi wa Leningrad waliendeleza mapambano ya ukombozi hadi Januari mwaka 1944, wakati walipofanikiwa kujiondoa katika mzingiro wa wanajeshi wa Ujerumani

No comments:

Post a Comment