Monday, 8 September 2014

upizani wa vyama vya siasa nchini Kongo juu ya kufanyiwa marekebisho katibaupizani wa vyama vya siasa nchini Kongo juu ya kufanyiwa marekebisho katiba



·          

Kwa mara nyingine tena chama cha 'Mrengo wa Kitaifa kwa ajili ya Marekebisho' nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kimesisitiza kuwa hatua ya kuifanyia marekebisho ya katiba ya nchi hiyo ina maana ya kuibua machafuko nchini. Viongozi wa chama hicho kwa kushirikiana na vyama vingine vya upinzani nchini Kongo wamelaani njama zozote za kutaka kutekeleza jambo hilo. Kabla ya hapo chama kilichoungana na chama tawala cha 'Wananchi kwa ajili ya Marekebisho na Demokrasia' kilitangaza azma ya kuifanyia marekebisho katiba ya Kongo. Kwa mujibu wa habari, marekebisho hayo yatahusu kipengee cha 220 ambapo ikiwa hatua hiyo itaungwa mkono na wananchi katika kura ya maoni, basi itatoa fursa kwa Rais Joseph Kabila kugombea kwa mara ya tatu katika uchaguzi mkuu ujao. Rais Kabila ambaye alichukua uongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuuawa baba yake Laurent-Désiré Kabila hapo mwezi Juni mwaka 2001, alishinda katika uchaguzi wa mwaka 2006 na 2011.
mjusi blogspot.com Katika safari yake nchini Marekani mwezi Agosti mwaka huu na katika kikao na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, John Kerry, Rais Kabila hakuweza kutoa jibu lililo wazi alipoulizwa na Kerry kuhusu azma yake ya kuifanyia marekebisho katiba. Tangu aliposhika madaraka ya nchi, Joseph Kabila amekuwa muitifaki mkubwa wa Marekani katika eneo la Maziwa Makuu ya Afrika. Kwa mujibu wa weledi wa mambo, kuanguka dikteta Mobutu Sese Seko hapo mwaka 1997, kulikuwa ni pigo kubwa kwa Ufaransa, na ushindi muhimu kwa Marekani. Hivi sasa John Kerry, amemtaka Rais Kabila achunge kanuni za demokrasia nchini mwake. Pamoja na yote hayo rais huyo kijana wa Kongo DRC hakuwa tayari kutoa jibu la wazi kwa Kerry. Suala hilo linaelezwa kuwa linatokana na Kabila kutaka kuwa na uhuru wa maamuzi na kupinga aina yoyote ya uingiliaji wa kigeni katika mambo ya ndani ya nchi yake. Itakumbukwa kuwa, mabadiliko ya Katiba ya Februari mwaka 2012 nchini Kongo DRC yalipelekea pia kutokea upinzani mkubwa wa vyama vya upinzani. Kwa mujibu wa vyama hivyo, mabadiliko hayo yalikuwa ni kwa maslahi ya chama tawala. Hivi sasa vyama vya upinzani na wakosoaji wa serikali ambao kwa pamoja waliunda muungano kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya katiba nchini humo, wamewataka wananchi kumiminika mabarabarani na kufanya maandamano makubwa hapo tarehe 13 mwezi huu. Weledi wa mambo wanayataja maandamano hayo tarajiwa kwamba yanaweza kuwa mwanzo wa upinzani wa wananchi  unaoungwa mkono pia na shakhsia wakubwa wa kisiasa nchini humo. Miongoni mwa shakhsia hao ni pamoja na mzee Etienne Tshisekedi ambaye ni mpinzani nambari moja wa Rais Kabila na mwenye wafuasi wengi nchini Kongo. Suala muhimu la kufaa kuzingatiwa ni kwamba, baada ya harakati za uasi wa wananchi zilizojiri katika nchi mbalimbali, harakati hizo zinaweza kuwaathiri pia Wakongomani na hivyo kuanzisha wimbi kubwa la uasi dhidi ya Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo

No comments:

Post a Comment