baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward
Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono.
Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama
cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka
38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya
chuo kikuu mwaka 1977.